Search This Blog

Wednesday 21 June 2017

IFAHAMU HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEPALIWA

IFAHAMU HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEPALIWA..

kupaliwa ni nini?
hii ni hali ya kukabwa na kitu kwenye koo ya hewa, inaweza kua chakula kitu chochote ambacho mtu alikua anakichezea mdomoni na hatimaye kikaenda kukwama kwenye koo la hewa.

ripoti ya shirika la afya duniani lilionyesha kwamba zaidi ya watu 162000 walifariki mwaka 2015 sababu ya kupaliwa na kukosa msaada wa haraka, idadi hiyo imetajwa kuongezeka muda unavyozidi kwenda lakini pia kupaliwa kunaweza kua hatari zaidi kwa watoto wadogo kwani anaweza kuweka kitu mdomoni na watu wakashindwa kujua kilichotokea.
mara nyingi watu hupaliwa na chakula, hela ya chuma, karanga, maharage,pini,kucha na kadhalika...                                                    

dalili za kupaliwa ni zipi?
mtu akipaliwa hua na dalili zifuatazo
kushindwa kuongea
kushindwa kupumua kawaida
kushindwa kukohoa
lips za mdomo kubadilika na kua blue sababu ya kukosa hewa
kupoteza fahamu.
                                         
utamsaidia vipi mtu aliyepaliwa?
mtu akipaliwa kama nilivyotaja hapo juu hushindwa kuongea, anaweza kuja kwako mbio bila kusema chochote akawa anakonyesha kwa vitendo tu lakini pia unaweza kua uliona wakati anapaliwa hivyo fanya vifuatavyo..
mpige ngumi au makofi matano mgongoni kwa nguvu lakini usitumie nguvu sana hasa kama ni mtoto, ukiona bado kitu hakijatoka simama nyuma yake kisha weka mikono yako kwenye tumbo la mgonjwa karibu na kifua kama picha inavyoonyesha hapo juu lisha vuta kwa ndani na kuachia mara tano kitaalamu kama heimlich manouver, lakini hii ya kuweka mikono tumboni mtoto awe na zaidi ya mwaka mmoja.
ukiona kitu kilichompalia kimetoka na mgonjwa hapumui mlaze chini kisha kandamiza kifua na kuachia kitaalamu kama cardio pulmonary resuscitation baada ya hapo mgonjwa apelekwe hospitali kuangalia kama kuna madhara yeyote ameyapata.
                                                         
                                                   
mwisho; huduma hiyo ya kumsaidia mgonjwa inatakiwa ifanyike haraka baada ya mgonjwa kukabwa kwani kukosa kwa hewa ndani ya dakika tano huweza kuleta kifo, lakini pia ukipata elimu hii wafundishe jamaa zako na ndugu zako kwani ukipaliwa wewe hutaweza kujisaidia.

2 comments:

  1. After having a persistent cough for over a year, I was diagnosed with COPD
    in March 2015. In 2016 my COPD got worse to the point where not only do I
    have trouble sleeping at night, I also struggle to get air into my lungs. I
    read in a health forum of a herbal centre (native health clinic) who have successful treatment to COPD/Emphysema, i immediately
    contacted the herbal centre via their website and purchased the COPD herbal
    remedy, I used the remedy for 2 weeks, all my symptoms were reversed, i did
    another test for confirmation, i was declared COPD free. email (
    nativehealthclinic@gmail.com) or WhatsApp/Call him on +2348140073965

    ReplyDelete
  2. The best herpes remedy, email [robinsonbucler@] gmail com

    ReplyDelete