Search This Blog

Friday 5 August 2016

VYAKULA VINAVYOONDOA MAUMIVU WAKATI WA HEDHI KWA WANAWAKE.


KILA mwanamke hupitia hatua ya kupatwa na hedhi mara moja kwa mwezi, ikiwa ni maumbile ya kawaida waliyoumbwa nayo. Lakini wanawake wengi husumbuliwa na matatizo kadhaa siku chache kabla au wakati wa siku zao, matatizo hayo hutofautiana kati ya mtu na mtu kutegemeana na afya ya muhusika.

DALILI ZA MATATIZO YA HEDHI
Siku chache kabla ya hedhi, baadhi ya wanawake hupatwa na hofu na huwa wenye hasira. Husumbuliwa na mfadhaiko wa akili, huumwa na kichwa, matiti hujaa maziwa, hukosa usingizi na kuvimba sehemu za siri. Hali hii husababishwa na kukosekana kwa uwiano wa homoni (Homone imbalance) na hali hii huweza kukoma ndani ya saa 24 baada ya kuanza hedhi.

MAUMIVU MAKALI YA HEDHI
Wengine hupatwa na maumivu makali sana wakati wa hedhi. Maumivu hayo huwapata akina mama ama siku mbili ama tatu kabla au mara tu waanzapo siku zao. Hali hii pia inasababishwa na kutokuwepo kwa uwiano wa homoni mwilini, ambako kumesababishwa na ukosefu wa virutubisho fulani.
Wengine hutokwa na damu nyingi kuliko kawaida au kukaa katika siku za hedhi kwa kipindi kirefu kuliko kawaida. Kuna sababu nyingi zinazoweza kuchangia hali hii, ikiwemo kuugua kwa muda mrefu, kupatwa na hofu, huzuni, mshtuko na sababu nyingine za kitabibu.


JUISI YA MBOGA ZIFUATAZO HUTIBU
Kwa kutumia vyakula asilia unaweza kuepukana na maumivu ya mara kwa mara wakati wa siku zako. Katika orodha ndefu ya juisi za mboga zinazotibu kwa uhakika matatizo yote ya hedhi, ni Kotimiri (Parsley), mboga ya majani ambayo upatikanaji wake ni rahisi. Kwa mujibu wa watafiti, Kotimiri ina uwezo wa kurekebisha uwiano wa homoni hivyo kuondoa matatizo kadhaa ya hedhi.

Inaelezwa kuwa uwezo wa Kotimiri kurekebisha matatizo ya hedhi unatokana na kuwa na aina ya kirutubisho kiitwacho ‘Apiol’ ambacho pia kimo miongoni mwa homoni za jinsia ya kike (estrogen). Maumivu na mvurugiko wa siku hurejea katika hali ya kawaida kwa kunywa juisi ya Kotimiri mara kwa mara.
Aidha, juisi hiyo inapochanganywa na juisi ya viazi pori (Beet Root), karoti au matango huwa na nguvu zaidi. Kiwango kinachoshauriwa kuchanganya kiwe na ujazo sawa kwa kila aina ya juisi utakayochanganya. Juisi yenye mchanganyiko huo ni rahisi kutengeneza na ni dawa inayoweza kumsaidia mwanamke wakati wote wa maisha yake bila kuhitaji kutumia dawa zingine kali za kuzuia maumivu (pain killers) ambazo huwa na madhara baadaye.

 
TANGAWIZI NAYO HUTIBU
Tangawizi nayo ni dawa nzuri sana ya kutibu matatizo yatokanayo na hedhi, hasa katika tatizo la maumivu makali na kutokupata hedhi. Chukua kipande cha tangawizi mbichi, kiponde na kiweke kwenye kikombe cha maji ya moto kwa dakika chache, kisha tia sukari kiasi na unywe mchanganyiko huo, kwa siku mara mbili kila baada ya mlo.

  UFUTA NAO NI DAWA
Ufuta (Sesame) nao ni miongoni mwa mbegu za asili unazoweza kula na kutibu matatizo ya hedhi. Saga ufuta na pata unga wake kisha uchanganye na maji ya moto, kunywa mara mbili kwa siku. Kinywaji hiki huondoa maumivu wakati wa hedhi kwa wasichana wadogo.

Ukitumia mara kwa mara kinywaji hiki cha ufuta, hutibu pia tatizo la kupata hedhi kidogo. Pia unaweza kuchangaya maji ya kuoga ya uvuguvugu na mbegu za ufuta zilizopondwa pondwa kiasi cha kiganja kimoja, nayo hutoa nafuu kubwa kwa wanaosumbuliwa na maumivu, hasa ukitumia siku mbili kabla ya siku zako.

PAPAI NALO NI DAWA
Papai bichi nalo linaelezwa na watafiti wetu kuwa lina uwezo wa kulainisha misuli ya njia ya uzazi hivyo kufanya utokaji wa hedhi kuwa mwepesi usio na maumivu. Papai huwa na manufaa zaidi kwa wasichana haswa kwa wale wenye tatizo la kutopata siku zao kutokana na kuwa na ‘stress’ au mawazo. Utapata faida hiyo kwa kula mara kwa mara tunda hilo bichi (ambalo halijaiva lakini limekomaa  

Prepared by Dr Salim Amour
          Cardio_thoracic surgeon

    


FAIDA 48 ZA JUISI YA TANGAWIZI AMBAZO ULIKUWA HUZIJUWI BADO

Huwa inanishangaza sana ninapoutafakari ukuu wa Mungu kwa namna ambayo ametupa mimea mbalimbali mhimu kwa ajili ya afya zetu – Mwanzo 1:29. Maelezo yafuatayo kuhusu tangawizi  yatakupa wewe ujuzi wa mmea mwingine wa asili usio na madhara ya kikemikali na kusaidia mwili wako kuwa na afya nzuri na ya kupendeza.

Tafiti mpya zinazidi kuonyesha namna mmea huu ulivyo wa mhimu kwa afya ya binadamu ikihusisha uwezo wake wa kudili na aina mbalimbali za kansa mwilini na tafiti nyingine zinaendelea kufanyika.

Tangawizi inaweza kuwekwa karibu kwenye kila chakula, iwe ni katika kuilainisha nyama nyekundu, kuongeza radha katika nyama au samaki, kama chai, kwenye juisi na kadharika. Binafsi napenda ikiwa kwenye juisi ya matunda ndiyo inakuwa tamu zaidi na inaenda kufanya kazi mwilini haraka zaidi.

Tangawizi ni zao la kibiashara na ni rahisi kutoka kimaisha kama utaamua kulima tangawizi ingawa ni zao la miezi mingi lakini ukivumilia utakula bata tu, gunia moja linauzwa kati ya laki 3 hadi 6 wakati wa msimu mzuri.

Tangawizi iliorodheshwa kwa mara ya kwanza na serikali ya Marekani kama dawa kwa ajili ya binadamu kati ya mwaka 1820 na 1873.

Tangawizi huongezwa pia katika vinywaji vingi vya viwandani zikiwemo soda ili kupata radha nzuri zaidi.

Leo nimekuletea hii juisi ya tangawizi, nimetumia tangawizi mbichi za ukubwa wa kati nne, parachichi moja na asali mbichi vijiko vikubwa saba na na maji lita moja na nusu.

Kazi 48 za tangawizi mwilini

1. Huondoa sumu mwilini haraka sana

2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi

3. Kuna viua vijasumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi

4. Huondoa uvimbe mwilini

5. Huondoa msongamano mapafuni

6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake

7. Huondoa maumivu ya koo

8. Huua virusi wa homa

9. Huondoa maumivu mbalimbali mwilini

10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills)

11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.

12. Tangawizi ina kiinilishe mhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”

13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-related cancer)

14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)

15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)

16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kanza mbalimbali za tumbo

17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi
18. Hutibu kanza za kwenye kizazi na kanza za kwenye mirija ya uzazi

19. Huongeza msukumo wa damu

20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo

21. Huzuia damu kuganda

22. Hushusha kolesto

23. Husafisha damu

24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa

25. Hutibu shinikizo la juu la damu

26. Husafisha utumbo mpana

27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma

28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI

29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula

30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu

31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu

32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa

33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula

34. Husaidia kuzuia kuharisha

35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu

36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto

37. Hutibu homa ya kichwa

38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi

39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito

40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis)

41. Huimarisha afya ya figo

42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi

43. Ina madini ya potassium ya kutosha

44. Ina madini ya manganese ambayo ni mhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali, hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita

45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha

46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium

47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene

48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita

Like ukurasa huu wangu kwa makala nyingine kali kama hii

Thursday 4 August 2016

DALILI 10 ZA KUSHIKA MIMBA


Dalili kumi za kukujulisha kuwa umeshika
mimba
Hutokea mara nyingi kina mama na wasichana
kuwa na kipindi cha msongo wa mawazo pale
wanapokosa siku zao na hasa kama
hawakutumia njia ya uzazi wa mpango au
kinga nyingine ya kushika mimba.
Kukosa siku zako sio dalili pekee ya kushika
mimba, bali kuna dalili zingine utalazoziona.
Kuna sababu nyingine nyingi zinazoweza
kukufanya ukose siku zako, hivyo soma dalili
za mimba ili ikusaidie kupata uhakika.

Moja, ni mabadiliko katika siku zako. Hii
kitaalamu tunaita spotting. Unaweza kushika
mimba ukaendelea kuona damu mwezi huo. Hii
hutokea yai lililorutubishwa linapojipandikiza
kwenye kizazi. Mishipa ya damu iliyojaa
kwenye ukuta huu tayari kulisha kiumbe
huachia damu kidogo amabazo mwanamke
anaweza kufikiri ni hedhi yake ya kawaida.
Hata hivyo mabadiliko yataonekana kwani
kiwango na siku za damu hubadilika.

Pili, ni kuongezeka ukubwa na kupata maumivu
kwenye maziwa. Hii inasababishwa na ongezeko
la homoni za istrogen pale unapokuwa umeshika
mimba. Hali hii huisha katika kipindi cha miezi
mitatu ya kwanza.

Tatu, ni kichefuchefu na kutapika. Hali hii
huwa mbaya zaidi wakati wa asubuhi
unapoToka kulala. Hii ni kwa sababu ya homoni
ya ‘projestroni’ ambayo husababisha
kupungua nguvu kwa misuli ya mrija wa
chakula au koromeo.

Nne, ni uchovu usiokuwa na usingizi usiokuwa
na sababu. Hii hutokea kwa sababu ya ongezeko
la homoni ya ‘projestroni’ na mama utajikuta
unasinzia mara kwa mara. Hali hii huisha
unapoanza mwezi wa nne wa mimba ila hata
kipindi cha mwisho wa mimba hujisikia uchovu.

Tano, kusumbuliwa na harufu mbalimbali. Hasa
kama unapata mimba kwa mara ya kwanza,
utachukia harufu za vyukula na vinywaji
mabalimbali. Wakati mwingine hata harufu za
watu walio karibu nawe zinaweza kukukera.

Sita, ni kujaa gesi tumboni. Utaona baadhi ya
nguo zako zinakubana zaidi hasa sehemu ya
tumbo. Hii ni kwa sababu ya homoni nyingi
mwilini zinazokufanya kijisikia tumbo kujaa.

Saba, Kukojoa mara kwa mara. Hii kwanza
hutokana na kuwa na damu nyingi mwilini
ambayo huongezwa na homoni za ujauzito
makusudi kutoa rishe ya kutosha kwako na kwa
kiumbe tumboni. Ukiwa na damu nyingi pia
utakojoa sana za kikemia mwilini. Pili
utajisikia kwenda haja ndogo mara nyingi pale
kiumbe kitakapoongezeka na kubana kibofu cha
mkojo.

Nane, kuongezeka kwa joto la mwili. Kwa kina
mama ambao hupima joto lao kama njia ya
uzazi wa mpango, watagundua kuwa joto
limepanda kwa muda wa wiki mbili au mbili na
nusu mfurulizo.

Tisa, kutoona siku sako kabisa. Kwa wale ambao
siku zao hazibadiliki na huenda vizuri
yawezekana kugundua pale wanapokose siku
nap engine kukimbilia hospitali. Hata hivyo kwa
wale ambao siku zao hubadilika sana wataona
kawaida ila kama ameshika mimba taona
mchanganyiko wa kichefuchefu, uchovu na
kusinzia pamoja na kukojoa mara kwa mara.

Kumi, kupima mkojo kwa kutumia kipimo cha
karatasi ngumu. Famasi nyingi huuza vipimo
ambavyo ikikichovya kwenye mkojo wako huweza
kugundua homoni za mimba kwenye mkojo.
Hii unaweza kupima mwenyewe ukiwa nyumbani
hata kazini. Kipimo hiki ukisha kichovya kwenye
mkoja kama katatsi inavyoelekea utaona
mistali baada ya dakika moja inajitokeza
upande wa chini.
Ikitokea mistari miwili basi unaweza kuwa na
mimba na ukitokea mmoja utakuwa huna
mimba. Kilingana na kiwango cha homoni
mwilini, kuna kina mama hakionyeshi majibu
mpaka upitishe wiki moja bila kuona siku zako.

Pamoja na dalili hapo juu, unatakiwa kupata
ushauri wa kitaalamu kutoka kwa daktari.  

Prepared by Dr Salim Amour
       Cardio_thoracic Surgeon

HEDHI NA MZUNGUKO WAKE



NINI MAANA YA MZUNGUKO WA HEDHI???
mzunguko wa hedhi ni mzunguko wa kila mwezi ambao husababisha kutokwa kwa damu ukeni kutokana na mimba kutotungwa,

Wednesday 3 August 2016

Tuesday 2 August 2016

HIZI NDIO FAIDA ZA KUNYWA MAJI GLASS SABA MWILINI



Suala la kunywa maji tumekuwa tukihimizwa kila mara na wataalamu wa Afya. Lakini zoezi hili limekuwa gumu kwa kuwa watu wengi huona kama adhabu. Imekuwa ikihimizwa angalau kunywa Lita mbili(2) za maji kila siku kwa kila mtu.
Nimekuwa nikiwasikia watu wengi wakidai wameenda Hospitali kutibiwa wameambiwa wanywe maji ya kutosha ili yawasaidie. Pia wengine wakithubutu kusema kuwa ukinywa maji mengi basi waweza tibu ugonjwa wa UTI kirahisi kabisa. Hili ni kweli lakini tatizo watu wengi hatuwezi kunywa hayo maji mengi.
Leo nitakupa mpangilio rahisi kabisa wa kunywa maji glass 7 kwa siku na faida zake mwilini. Hii itakusaidia zaidi maana glass 7 ni sawa na Lita 2 karibu na nusu.

GLASS 1. kunywa maji glass moja mara baada ya kuamka. Hii husaidia viungo vya ndani vya mwili kama figo, moyo, n.k

GLASS 1. Nusu saa kabla ya kunywa chai. Husaidia katika mmeng'enyo wa chakula

GLASS 1. Kabla ya kuoga asubuhi. Husaidia kushusha shinikizo la moyo

GLASS 1. Nusu saa kabla ya chakula cha mchana. Pia husaidia katika mmeng'enyo wa chakula

GLASS 1. Kabla ya kuoga jioni. Pia husaidia kushusha shinikizo la moyo

GLASS 1. Nusu saa kabla ya chakula cha usiku. Vilevile husaidia katika suala la mmeng'enyo wa chakula

GLASS 1. Kabla ya kulala. Husaidia kuepuka kupata shambulio la moyo
Hiyo ndiyo ratiba nzuri ya kunywa maji glass 7 bila kuhangaika.

MASUNDOSUNDO (GENITAL WARTS )

TIBA YA UGONJWA WA KUOTA KINYAMA SEHEMU ZA SIRI NA SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI (GENITAL WARTS & SKIN) 

HEMORRHOIDS {BAWASIRI)

TIBA SAHIHI YA UGONJWA WA BAWASIRI AU KUOTA KINYAMA SEHEMU YA HAJA KUBWA IMEPATIKANA!!!

CONSTIPATION {UKOSEF WA CHOO KWA MUDA MREF)

UGONJWA WA KUKOSA CHOO KWA MUDA MREFU {CONSTIPATION}
Ugonjwaa huu kitaalam tunaita constipation
mtu hukosa choo siku tatu au mpaka wiki nzima na akipata basi ni kidogo sana na kikavu mpaka anakua akiskia maumivu