Search This Blog

Wednesday 3 August 2016

UTI

UGONJWA WA UTI (WANAWAKE)

MAAMBUKIZI KATIKA NJIA YA MKOJO
(URINARY TRACT INFECTIONS)
 Ugonjwa wa maambukizi katika njia ya mkojo (uti)_ugonjwa huu ni common hususani kwa wanawake ambapo ugonjwa huu huwashambulia sana kutokana na maumbilee yao kila wanapokwenda msalani kwani huwabidi kuchuchumaa na kuambukizwa kwa urahisi

 ugonjwa huu umekua ukipuuziwa na baadhi ya wanawake na kuona ni wa kawaida hauna madhara makubwa na hivyo hawachukulii maanani kupata matibabu vizuri 

FAHAMU VIZURI KUHUSU UTI 
UTI_ni maambukizi katika sehemu yoyote ya njia ya mkojo husababisha maradhi au magonjwa ya aina mbalimbali kama vile UTI, FANGASI UKENI 
ugonjwa huu huweza kumpata mtu yoyote Bila kujali jinsia au umri hata hivyo yapo pia Makundi ambayo kutokana na sababu za BIOLOGY na Kinga ya mwili kushuka au kuwa ndogo huathiriwa Zaidi na ugonjwa huu wa uti, Makundi hayo ni WATOTO, WAZEE NA WANAWAKE
A) WATOTO ~Hawa ni waathirika wakubwa wa UTI na yaweza kusababisha maambukizi kusambaa hadi katika damu mwilini na kusababisha KIFO 

B) WANAWAKE ~wao huathiriwa Zaidi na uti hasa kutokana na mfumo mzima wa maungo yao hasa ya mfumo wa mkojo kuwa na urahisi wa kuingiliwa na bacteria, mathalani mrija wa mkojo yan URETHRA ya mwanamke ni fupi sana ukilinganisha na ya mwanaume na hivyo vijidudu au bacteria kupata urahisi wa kuingia ndani

 UKUBWA WA TATIZO
 Kwa kiasi kikubwa tatizo la uti huathiri wanawake Zaidi kuliko wanaume Zaidi ya Mara mbili kwa kukadiria, karibu kila mwanamke katika maisha yake anaweza kupata uti pia uwezekano wa tatizo kujirudia Mara kwa Mara kutokana na mazingira wanayoishi na ubaya wa pedi wanazotumia 

VIHATARISHI 
sababu hatarishi za uti Zipo nyingi kulingana na umri na jinsia na mazingira ya mhusika MFANO sababu hatarishi za mtoto mchanga kupata uti si Sawa na mtu mzima jinsia ya kike yote hii ni kwasababu maumbilee na mfumo wa mwanamke humweka katika nafasi nzuri ya kupata uti vilevile ngono Tena ya Mara kwa Mara husababisha maambukizi ya UTI pia sababu nyingine ni upungufu wa Kinga mwilini kwa sababu yoyote ikiwamo UJAUZITO KWA WANAWAKE au UGONJWA WA KISUKARI
VISABABISHI VYA UTI 
 Uti yaweza kusababishwa na vijidudu vya namna nyingi, mathalani ni vimelea (bacteria) japo pia na jamii nyingine ya vijidudu vinaweza kusababisha UTI. Pia bacteria aina ya ESCHERICHIACOL kwa kias kikubwa ndio vinavyosababisha UTI japo pia bacteria wengine wapo,vijidudu hivi vyaweza kuingia katika njia ya mkojo kutokea nje ya mwili au kupitia damu ya mhusika 
~kwa wanawake fangasi katika sehemu za siri imekua ni shida sana na kusababisha bacteria kuzaliana
 ~kwa wanaume Mara nyingi hutokana na maumbilee yao na mfumo mzima wa mkojo na viungo vyake hata hivyo huwa siyo waathirika wakubwa wa UTI
DALILI ZA UTI
 Dalili kwa kiasi kikubwa hutokana na umri na jinsia ya mhusika Lakin Zaidi kusababishi (cause) ya UTI, Dalili zinaweza kuwa
 👉KUSIKIA MAUMIVU WAKATI WA HAJA NDOGO 
 👉KUHISI HOMA NA MAUMIVU KATIKA VIUNGO VYA MKOJO
 👉KUHISI KUHITAJI KUKOJOA MARA KWA MARA
 👉MKOJO KUWA NA HALI YA KUUNGUZA
 👉MAUMIVU YA TUMBO CHINI YA KITOVU NA MGONGO KWA CHINI 
MATIBABU YA UTI NA JINSI YA KUJIKINGA ~matibabu ya UTI hupatikana kwa urahisi, Bila usumbufu wowote maadamu tatizo likijulkana mapema, utaratibu wa matibabu hutegemea na majibu ya maabara, kusababishi cha uti na umri wa mhusika, pia pamoja na hayo uti ni ugonjwa unaozuilika kwa ujumla, swala la kuzingatia ni kanuni za afya bora hasa ya USAFI hasa USAFI WA MWILI NA MAZINGIRA NI SULUHUSHO TOSHA KWA TATIZO LA UTI, pia unywaji wa maji mengi na JUICE YA MIWA husaidia kusafisha njia ya mkojo pia unashauriwa kukojoa Mara baada ya KUFANYA TENDO LA NDOA,
 ~PIA KWA WANAWAKE MNAPASWA KUTUMIA SABUNI YA ASILI INAYOITWA LADY INTIMATE WASH ILI KUJIKINGA NA MAGONJWA YA MAAMBUKIZI UKENI, PIA ZINGATIENI PADS ZA KUVAA PENDELEENI KUVAA PADS AINA YA NEPLILY ZENYE ANIONS KATIKATI PIA KWA WAZAZI ZINGATIENI PAMPERS KWA SABABU PAMPERS NYINGI HAZINA ALOIN YA KUMKINGA MTOTO NA MAGONJWA YA UTI NA FANGASI HIVYO MZAZI PAMPERS NZURI NI NEPBABY DIAPERS HIZO ZINA ALOIN NA INDICATOR INAYOONYESHA MTOTO WAKATI HUU AMEKOJOA HIVYO UNAPASWA KUMBADILISHA NA HIVYO MTOTO KUWA 
SALAMA 

 Prepared by Dr Salim Amour
          Cardio_thoracic surgeon

No comments:

Post a Comment