Search This Blog

Sunday 23 October 2016

TUNDU KATIKA MOYO WA MTOTO



Ugonjwa wa tundu katika moyo wa mtoto.

Image result for TUNDU KATIKA MOYO WA MTOTO
Kama kawaida safu hii huwa tunajadili masuala mbalimbali yanayohusu afya na tiba ili kupata ufahamu zaidi juu ya kuimarisha afya zetu na ya jamii kwa ujumla.
Leo tutazungumzia ugonjwa unaojulikana kama tundu katika kuta za ventrikali za moyo au kwa kitaalamu Ventricular Septal Defect (VSD).
Tatizo hili hutokea mara nyingi ambapo watoto 2-6 kati ya 1,000 uzaliwa nalo.
Tundu katika kuta za chini za moyo au VSD ni pale panapokuwepo na uwazi katika sehemu ya kuta ya septum inayotenganisha chemba za ventrikali zilizo chini ya moyo.
Moyo unapoanza kuumbika huanza kama bomba lililo wazi na kuendelea kujigawa katika sehemu mbalimbali na kuunda kuta.
Iwapo kitendo hicho hakitatekelezwa ipasavyo, hutokea uwazi katika kuta ya septum kwenye chemba za chini.
Kuwepo tundu hilo huruhusu damu yenye oksijeni kupita kutoka chemba ya kushoto ya chini ya moyo na kuingia katika chemba ya kulia ya chini ya moyo, badala ya kuingia kwenye mshipa wa aorta na kuelekea nje ya moyo kama inavyotakiwa.
Tundu la VSD linaweza kuwa dogo, la kati au kubwa. Tundu dogo katika kuta za chini za moyo huruhusu damu ndogo tu kutoka upande mmoja wa moyo kwenda wa pili hivyo haliathiri utendaji wa kawaida wa moyo na kwa kawaida huwa halihitaji matibabu maalumu.
Matundu ya aina hiyo huziba yenyewe wakati moyo unapoendelea kukua kipindi cha utotoni. Matundu yenye ukubwa wa kati na kubwa katika kuta za chini za moyo huruhusu kiwango kikubwa zaidi cha damu kupenya toka upande mmoja wa moyo kwenda mwingine, na mara nyingi huhitaji matibabu maalumu.
Watoto wenye tundu dogo katika moyo, huweza kukua bila matatizo yoyote, wakati wale wenye tundu kubwa huanza kuonyesha dalili mapema.
Vifuatavyo ni vihatarishi ambavyo vinaweza kusababisha mtoto kuzaliwa na tundu katika kuta za chini za moyo. Mama kuwa na maambukizi ya Rubella katika kipindi cha ujauzito au kuwa na ugonjwa wa kisukari cha wakati wa ujauzito ambao haujadhibitiwa na kuwa mnywaji wa pombe au mtumiaji wa madawa ya kulevya.
Mjamzito akitumia bila ushauri wa daktari baadhi ya dawa za hospitali katika kipindi cha ujauzito pia huweza kusababisha mtoto azaliwe na tundu katika kuta za chini za moyo.
DALILI
Iwapo tundu ni dogo huwa halina dalili yoyote na pale mtoto anapoendelea kukua tundu hilo hujifunga lenyewe. Lakini tundu likiwa kubwa, japokuwa mtoto anayezaliwa huwa haonyeshi dalili yoyote katika kipindi hicho lakini baadaye huwa na dalili zifuatazo.
Rangi ya ngozi yake, midomo na kucha hubadilika na kuwa ya bluu, kunyonya au kula huwa kwa shida sana, ukuaji na kupumua kwa shida, kuchoka haraka, kujaa miguu na kuvimba tumbo, kuwa na mapigo ya moyo ya haraka.
Mtoto mwenye tatizo hili anapopimwa na daktari kwa kifaa, huweza kusikia ishara ya ongezeko la sauti ya ziada ya mapigo ya moyo wa mtoto hali ambayo kitaalamu huitwa holosystolic murmur.

MATATIZO YA FIGO

Matatizo ya Figo na dalili zake.


VISABABISHI VYA UGONJWA WA FIGO
1.Matumizi mabaya ya dawa hasa za maumivu kama diclofenac na madawa mengine ya maumivu.
2.Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe kupita kiasi

KAZI ZA FIGO
1. Kuchuja vitu mbalimbali pamoja na sumu katika damu, kusaidia kuhifadhi,kudhibiti kiwango cha maji na madini (electrolytes) mwilini.
Figo huchuja vitu hivyo pamoja na maji yaliyo mwilini na kutengeneza mkojo, huchuja pia maji yasiyohitajika mwilini huku yakinyonya madini na kemikali muhimu kuzirudisha katika mzunguko wa damu na kutoa nje uchafu usiohitajika.
2. Kusaidia kutengeneza kiasili cha erythropoletin ambacho ni muhimu katika utengenezaji wa chembechembe nyekundu za damu, hupokea asilimia 25 ya damu na kila figo ina chembechembe hai ndogo milioni moja, pia kusaidia kudhibiti na kurekebisha shinikizo la damu mwilini (blood pressure).
AINA ZA UGONJWA WA FIGO.
Zipo Aina mbili za Ugonjwa wa figo

1.Aina ya `kwanza figo kushindwa kufanya kazi kwa ghafla na muda mfupi.
2. Aina ya pili ni ile ya figo kushindwa kufanya kazi polepole na kwa muda mrefu.Figo huharibiwa taratibu na kuendelea kupunguza uwezo wake wa kufanya kazi kadiri siku zinavyokwenda.Figo kushindwa kufanya kazi polepole na kwa muda mrefu.
SABABU ZA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI KWA GAFLA
1. Kupungua kwa mzunguko wa damu kwenye figo, kemikali za mwilini au kushambuliwa na sumu. Sababu za figo kushindwa kufanya kazi ghafla
2.Ugonjwa wa moyo, moyo kushindwa kusukuma damu kwa ghafla, au waliougua maradhi ya moyo kwa muda mrefu.
3.Sababu zinazofanya figo ishindwe kufanya kazi taratibu na kwa muda mrefu na hatimaye kushindwa kabisa kuwa ni presha kuwa juu, kisukari, magonjwa yanayosababishwa na bakteria, HIV, saratani na sumu mbalimbali zinazoingia mwilini.

DALILI ZA FIGO KUSHINDWA KUFANYA KAZI.
1.Dalili ya kwanza ni kupungua kwa kiasi cha mkojo, kushindwa kupumua, kusikia kichefuchefu, kutapika na kuvimba miguu.
2.Dalili nyingine ni maji kujaa mwilini, madini ya mwili kuwa juu hasa ya ‘potashiamu’, asidi nyingi, matatizo katika moyo, ubongo, kukosa hamu ya kula na kudhoofika mwili.
3. Dalili nyingine kwa wagonjwa ambao hawagunduliki mapema ni kuvimba macho wakati wa asubuhi na uvimbe kupungua baadaye.
4. Dalili nyingine ni kuvimba miguu asubuhi, kupungukiwa damu mwilini kama dalili za kwanza (kwani figo ikishindwa kufanya kazi ya kusaidia kutengeneza damu).
TAFADHALI SHARE NA WENGINE ILI ELIMU HII IWEZE KUWA SAIDIA

PROSTATE GLAND (TEZI DUME)


Hii ndiyo makala inayoelezea ugonjwa wa Tezidume.

Image result for tezi dume in english
Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili, lobes, ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu. Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).
Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la ngono. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Aidha majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya fallopian tayari kwa utungisho na yai la kike. Vilevile
husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo kama isiporekebishwa, huweza kuua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu.

Kuvimba Tezi Dume (BPH)
Kwa kadiri mwanaume anavyozeeka, ni jambo la kawaida pia kwa tezi dume kuongezeka ukubwa na kuvimba. Hali hii kitabibu huitwa Benign Prostate Hyperplasia au wengine hupenda kutumia maneno Benign Prostate Hypertrophy kwa kifupi BPH. Kwenye makala hii tutautumia sana ufupisho huu wa BPH ili kurahisisha mambo.
Ukuaji wa tezi dume hupitia hatua kuu mbili. Hatua ya kwanza hutokea kipindi cha balehe wakati tezi dume linapoongezeka ukubwa na kuwa mara mbili ya lilivyokuwa hapo awali. Baada ya hapo ukuaji husimama kwa muda mpaka kijana anapofikisha miaka 25 hadi 30 ndipo hatua ya pili ya ukuaji huanza tena. Ukuaji huendelea kwa viwango na kasi tofauti kati ya mtu na mtu na hatimaye kusababisha BPH katika umri wa utu uzima.
Wakati tezi dume linapokua na kutanuka, utando wa tishu unaozulizunguka hutanuka pia. Hata hivyo ingawa tezi dume huendelea kukua, hufikia wakati utando wake huacha kutanuka na kufanya tezi dume kubana mrija wa kutolea mkojo kutoka kwenye kibofu. Hali hii husababisha kibofu cha mkojo kuwa na ngozi ngumu. Hali hii hufanya kibofu cha mkojo kuhisi kutaka kutoa mkojo nje hata kama kiasi cha mkojo ndani yake ni kidogo sana. Hufikia wakati, kibofu huwa dhaifu na kupoteza uwezo wake wa kuhisi kutoa mkojo na hivyo kufanya mtu anapokojoa kushindwa kutoa mkojo wote na badala yake hubakiza kiasi fulani cha mkojo kwenye kibofu.

BPH husababishwa na nini?
Chanzo halisi cha BPH au vihatarishi vyake (risk factors) havijulikani kwa uhakika. Kwa muda mrefu imekuwa ikichukuliwa kuwa BPH hutokea kwa wanaume watu wazima na wazee tu. Aidha imewahi kuonekana huko nyuma kuwa PBH haitokei kwa wanaume ambao wamewahi kufanyiwa operesheni ya kuondoa korodani au wale ambao walizaliwa bila korodani. Hali imepelekea baadhi ya watafiti kuamini kuwa BPH ina uhusiano mkubwa na umri wa mtu pamoja na uwepo wa korodani.
Kuna dhana (theories) kadhaa zinazojaribu kuelezea chanzo cha BPH. Dhana hizo ni pamoja na
  1. Uhusiano kati ya BPH na homoni ya estrogen: Wanaume huzalisha testosterone, homoni ya muhimu sana katika mwili wa mwanaume. Hali kadhalika huzalisha pia estrogen ambayo ni homoni ya kike kwa kiwango kidogo sana. Kadiri jinsi mtu anavyozeeka, ndivyo uzalishaji wa testosterone unavyokuwa mdogo na kufanya kiwango chake katika damu kupungua kulinganisha na kiwango cha estrogen ambacho huongezeka kwa kiasi fulani. Pamoja na kazi nyingine, estrogen pia huchochea ukuaji wa chembe hai za mwili. Tafiti zilizofanywa kwa wanyama zimeonesha kuwa BPH hutokea kwa sababu kiwango kikubwa cha estrogen katika damu huchochea ukuaji wa seli za tezi dume na hivyo kufanya tezi dume kuvimba.
  2. Uhusiano kati ya BPH na Dihydrotestosterone (DHT): DHT ni kiasili kinachozalishwa kutokana na testosterone kwenye tezi dume, ambacho husaidia kuthibiti ukuaji wa tezi dume. Ingawa wanyama wengi hupoteza uwezo wa kuzalisha DHT wanapofikia umri wa uzee, baadhi ya tafiti zimeonesha kuwa, kwa binadamu, hata kama kiwango cha testosterone kitapungua sana katika damu, wanaume watu wazima bado wana uwezo wa kuzalisha kiasili hiki cha DHT katika tezi dume zao. Uzalishaji na uklimbikaji huu wa DHT huchochea kwa kiasi kikubwa ukuaji wa seli za tezi dume na kusababisha BPH. Wanasayansi wamegundua kuwa wanaume watu wazima wenye kiwango kidogo cha DHT hawapati BPH.
  3. Uhusiano kati ya BPH na maelekezo ya seli: Dhana nyingine inasema kwamba baadhi ya seli kutoka katika sehemu fulani ya matezi yanayohusika na ukuaji mwilini hupewa maelekezo wakati mtu anapokuwa bado mdogo. Seli hizi hutunza maelekezo hayo na baada ya miaka kadhaa maelekezo haya huanzwa kutekelezwa na seli za matezi mengine. Mojawapo ya melekezo hayo ni kuchochea ukuaji wa tezi dume na kusababisha BPH.

Dalili za BPH
Dalili za BPH hutokea kwa sababu ya kubanwa kwa njia ya kutoa mkojo nje ya mwili (urethra) au kibofu kushindwa kuthibiti mkojo. Aidha dalili hizi hutofautiana kati ya mtu na mtu, ingawa karibu wagonjwa wote
  1. Hukojoa mkojo unaokatika katika
  2. Hukojoa mkojo wenye mtiririko dhaifu
  3. Husita kabla ya kuanza kukojoa
  4. Hali ya kujihisi kubanwa na mkojo kila mara
  5. Kushindwa kuthibiti mkojo kiasi cha mkojo kutirika wenyewe
  6. Hali ya kuhisi mkojo haujaisha kwenye kibofu
  7. hukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku
  8. Kushindwa kukojoa kabisa (urine retention)
  9. Au dalili zinazotokana na madhara ya BPH

Madhara ya BPH
BPH kama ilivyo saratani ya tezi dume, inaweza kumletea mgonjwa madhara (complications) kadhaa. Madhara hayo ni pamoja na
  1. Mkojo kushindwa kutoka (retention of urine)
  2. Mgandamizo kwenye kibofu cha mkojo
  3. Vijiwe kwenye kibofu cha mkojo
  4. Uambukizi katika njia ya mkojo (UTI)
  5. Madhara katika figo au kibofu
  6. Shinikizo la damu
  7. Kushindwa kutoa shahawa kwenye uume (retrograde ejaculation)
  8. Maambukizi mbalimbali
  9. Nimonia (Pneumonia)
  10. Damu kuganda
  11. Uhanithi

Vipimo na Uchunguzi
Baada ya mgonjwa kujihisi dalili zilizotajwa hapo juu, daktari atamfanyia uchunguzi wa mwili kabla ya kumfanyia vipimo zaidi. Vipimo vyaweza kutofautiana kati ya mgonjwa namgonjwa, lakini baadhi ya vipimo ni pamoja na
  1. Kuchunguza Tezi Dume kupitia njia ya haja kubwa au Digital Rectal Examination (DRE): Hiki ni kipimo cha kwanza kabisa ambacho mgonja hufanyiwa na daktari wake. Ni kipimo kinachoweza kumpa daktari picha ya tatizo na kufahamu kuhusu ukubwa na hali ya tezi dume. Daktari akiwa amevaa glovu huingiza kidole chake cha shahada katika njia ya haja kubwa au puru (rectum) ya mgonjwa kasha kuzungusha zungusha ili kufahamu kama tezi limevimba ama la na pia hali yake kama ni gumu kuliko kawaida ama lina utando na nyama laini.
  2. Kipimo cha damu cha Prostate-Specific Antigen (PSA): PSA husaidia kutofautisha kati ya saratani ya tezi dume na BPH. PSA ni aina ya protein inayozalishwa na seli za tezi dume na kiwango chake huongezeka iwapo kuna saratani ya tezi dume.
  3. Utrasound ya Puru (Rectal Ultrasound): Kipimo hiki hufanyika iwapo daktari atahisi kuwepo kwa saratani ya tezi dume badala ya BPH. Utrasound ya puru pamoja na kuonesha taswira ya tezi dume ilivyo, pia humuwezesha daktari kuchukua kinyama (biopsy) kwenye tezi dume kwa ajili ya uchunguzi zaidi ili kutofautisha kati ya saratani na BPH.
  4. Kiwango cha utokaji wa mkojo (Urine Flow Study): Ni kipimo kinachotumika kufahamu kasi ya utokaji wa mkojo. Mkojo unaotoka kwa kasi na kiwango kidogo huashiria kuwepo kwa BPH.
  5. Kipimo cha kuchunguza kibofu cha mkojo (Cystoscopy): Kipimo hiki husaidia kuweza kufahamu ukubwa wa tezi, sehemu tezi lilipobana njia ya mkojo na kiwango cha kubana huko. Aidha huwezesha pia kutambua hali ya kibofu cha mkojo ikoje.

Matibabu

Matibabu ya BPH yameganyika katika sehemu mbili, yale yanayofanywa kwa kutumia dawa na yale yanayofanywa kwa kutumia upasuaji mdogo. Aidha matibabu hufanywa kwa watu wenye BPH kubwa zaidi na dalili zinazowaletea usumbufu na kuathiri maisha yao, wakati wale wenye dalili ndogo ndogo hawalazimiki sana kuhitaji matibabu.

Matibabu kwa njia ya dawa
Dawa hizi hutumika kwa lengo la kulifanya tezi dume kusinyaa na kupungua ukubwa wake. Dawa hizo ni pamoja na
  • Finasteride na dutasteride ambazo huzuia uzalishajiwa homoni ya DHT. Matumizi ya dawa hizi husaidia kuzuia kukua na kuvimba kwa tezi dume au kulifanya tezi dume kusinyaa kabisa kwa baadhi ya wanaume.
  • Terazosin, doxazosin, tamsulosin na alfuzosin husaidia kulainisha misuli ya tezi dume na hivyo kupunguza mbano wa mrija wa urethra, hali inayosaidia mkojo kutoka vizuri.

Matibabu kwa njia ya Upasuaji

Upasuaji mdogo (minimal Invasive procedures)
Upasuaji mdogo husaidia kuondoa dalili za BPH na hufanyika pale ambapo matibabu kwa njia ya dawa yameshindwa kuonesha mafanikio yeyote. Njia hizo ni
  • Tiba ya kutumia mawimbi ya joto (Transurethral microwave procedures, TUMT): Tiba hii hutumia kifaa kinachotoa mawimbi ya joto (microwave) yanayochoma na kuharibu tishu zilizovimba za tezi dume. Matibabu huchukua chini ya saa moja na yanaweza kufanyika bila mgonjwa kuhitaji kulazwa.
  • Tiba ya kutumia sindano maalum (Transurethral needle ablation, TUNA): Njia hii hutumia visindano vidogo ambavyo huunganiswa kwenye chombo chenye kutoa nishati ya joto kuunguza tishu zilizovimba za tezi dume.
  • Tiba ya kutumia joto la maji (Water-induced thermotherapy): Tiba hii hutumia maji ya moto yaliyochemshwa kwa kifaa maalum kuunguza na kupunguza tishu zilizovimba za tezi dume.
Upasuaji mkubwa
Madaktari wengi hushauri kuondolewa kabisa kwa tezi dume iwapo itathibitika kuwa mgonjwa ana BPH. Zipo njia nyingi za upasuaji wa BPH, nazo ni pamoja na upasuaji kwa kupitia kwenye mrija wa mkojo (Transurethral surgery, TURP), upasuaji mkubwa wa wazi (Open surgery), upasuaji wa kutumia nishati kuondoa tishu za tezi dume (Laser surgery), na upasuaji wa kutumia joto la fibreoptic probe kuchoma tishu za tezi dume (Interstitial laser coagulation).
Vitu vya kufanya baada ya Upasuaji wa Tezi dume
Mara baada ya upasuaji wa tezi dume inashauriwa
  • Kunywa maji kwa wingi ili kusafisha kibofu cha mkojo
  • Epuka kujikakamua sana unapojihisi kwenda haja kubwa
  • Kula lishe bora ili kuepuka kupata choo kigumu. Iwapo mgonjwa atapatwa na choo kigumu ni vyema amuone daktari ili amshauri jinsi ya kuondoa tatizo.
  • Epuka na acha kunyanyua vitu vizito.
  • Hairuhusiwi kuendesha gari wala kuendesha mtambo wowote ule mpaka utakapopona kabisa.
Matatizo yanayoweza kutokea baada ya upasuaji
  • Shida wakati wa kukojoa: Kawaida huchukua muda wa siku kadhaa mtu kuweza kurejea katika hali yake ya kawaida ya kukojoa.
  • Shida ya kuthibiti mkojo usitoke ovyo (Incontinence): Ni kawaida kwa mgonjwa kushindwa kuthibiti kutoka kwa mkojo katika siku za mwanzo baada ya operesheni. Hata hivyo hali hii hujirekebisha baada ya siku kadhaa kupita.
  • Kutokwa na damu: Katika siku za wali mara baada ya TURP, kidonda kwenye tezi dume kinaweza kuvuja damu ambayo itaonekana katika mkojo. Hta hivyo hali hii hukoma baada ya wiki kadhaa. Hata hivyo iwapo utokaji damu ni mzito sana, inashauriwa kumuona daktari haraka.

Uwezo wa kufanya ngono baada ya upasuaji
Wagonjwa wengi waliofanyiwa upasuaji wa BPH uhofia sana kuhusu uwezo wao wa kufurahia tendo la ngono mara baada ya upasuaji. Kwa kawaida, huchukua muda fulani kwa agonjwa kuweza kurejea hali ya kawaida ya kufurahia tendo hili.
  • Mdiso au kudindisha (Erections): Madaktari wengi husema kuwa iwapo mgonjwa aliweza kupata mdiso au kudinda muda mfupi baada ya upasuaji, uwezo wake wa kuendelea kupa mdiso ni mkubwa zaidi. Hata hivyo iwapo mgonjwa hakuwa na uwezo wa kudisa tangu awali, upasuaji wa tezi dume hauna uwezo wa kumrejeshea uwezo wake wa kudisa.
  • Kutoa mbegu (Ejaculation): Ingawa wanaume waliofanyiwa upasuaji wa tezi dume bado wanaweza kupata mdiso, mara nyingi upasuaji huu huwafanya wawe wagumba yaani wasioweza kupata watoto. Hali hii kwa kitaalamu huitwa retrograde ejaculation au kilele (mshindo) kikavu (dry climax). Kwa kawaida, wakati wa tendo la ngono, mbegu za kiume kutoka kwenye korodani huingia kwenye urethra karibu na kijitundu cha kibofu cha mkojo. Wakati wa tendo la ngono, misuli maalum hufunga kijitundu hicho ili kuzuia mbegu zisiingie kwenye kibofu badala yake zielekee kwenye urethra ya katika uume. Hata hivyo, upasuajiwa BPH huondoa misuli hiyo na kufanya mbegu kuingia kwenye kibofu cha mkojo badala ya kuendelea kwenye urethra ya uume. Shahawa hizo hatimaye hutolewa nje ya kibofu pamoja na mkojo.
  • Kufika kilele (Orgasm): Huwa hakuna tofauti kubwa ya kufika kilele (orgasm) kabla na baada ya kufanyiwa upasuaji.

BPH na Saratani ya Tezi Dume: Hakuna Uhusiano wa moja kwa moja

Ingawa baadhi ya dalili za BPH zinafanan na zile za saratani ya tezi dume, kuwa na BPH hakuongezi uwezekano wa kupata saratani ya tezi dume. Hata hivyo, mwenye BPH anaweza pia na saratani ya tezi dume bila saratani hiyo kugundulika, ama wakati huo huo au siku za baadaye. Hivyo inashauriwa kuwa, ni vema wanaume wote kuanzia miaka 40 na keundelea kufanya uchunguzi wa tezi dume zao walau mara moja kila mwaka.
Image result for tezi dume in english


Saturday 22 October 2016

Je wajua kuwa wanaume nao huingia katika hedhi?

Je wajua kuwa wanaume nao huingia katika hedhi?

Mara nyingi nimekua nikiamini kwamba yale tunayoyafahamu kuhusu maisha ni machache sana ukilinganisha na yale tusioyafahamu.
Kiasi cha miezi kadhaa iliyopita nilisoma utafiti fulani kuhusu hedhi. Awali nilipousoma niliona ni hadithi tupu.
Lakini nilipoona ni vyema kuujaribu kwa kutenda miezi minne baadae nilishangaa. Hata wewe najua utashangaa utakaposoma makala haya.
Lakini ombi langu kwako ni kukutaka ujaribu kufanya mazoezi ili uthibitishe ukweli huo.
Kikomo cha kuwa na hamu ya kufanya mapenzi kwa wanaume ni miaka 42. Hata wanawake ni hivyo hivyo.
Kama mwanamke ataruhusiwa kuwa na uhuru wa kufanya mapenzi kila wakati kama apendavyo bila kuzuiwa na mila na desturi kikomo cha kutokuwa na hamu ya kufanya mapenzi ni miaka 42.
Hakuna tofauti kati ya wanawake na wanaume. Miaka ya hivi karibuni imegundulika kwamba hata wanaume hupata hedhi-ingawa wanaume hawana alama za nje za kuwaonesha kwamba wako kwenye hedhi, kama walivyo wanawake ambao hutoka damu siku zao za hedhi zinapofika na kukamilika.
Kwa karne na karne hakuna mtu aliyekuwa akifikiria kwamba wanaume wangeweza kuwa wanapata nao hedhi kama wanawake.
Kama mwanaume akiamua kuweka kumbukumbu zake kwenye dayari na kujiangalia kila siku hali yake inavyobadilikana kuwa ya kusikitika, ya kawaida, furaha na hasira……akiifuatilia hali yake namna hiyo kwa siku zote 28 za mwezi, halafu na mwezi unaofuata, akafanya hivyo hivyo, halafu mwezi wa tatu nao akatenda hivyo, na halafu ailinganishe miezi hiyo mitatu atashangaa.
Kuna siku tatu, nne au tano ambazo zitafanana katika dayari zote tatu, lini ana hasira ana masikitiko, ni mharibifu, na tabia nyingine kama hizo. Hivyo ndivyo vipindi vya hedhi kwa wanaume kama ilivyo kwa wanawake.
Zoezi hili anaweza kufanya mwanaume yeyote, akishindwa kupata matokeo anaweza kuwasiliana na mtandao  huu kwa Utambuzi na Kujitambua na kuuliza ni kwa nini nimeandika uongo.
Ni jambo ambalo lipo na limeshafanyiwa tafiti mbalimbali, hata mimi binafsi nimefanya zoezi hilo kwa miezi minne na limetoa majibu kama hayo.
Kwa kawaida mwanaume hana dalili za kimwili za kutoka damu kama mwanamke – ndio maana, karne na karne hakuna mtu aliyejali – lakini ni jambo la uhakika kwamba wanaume wanapata hedhi.
Dalili za mwanaume aliye kwenye hedhi ziko akilini zaidi na sababu ziko wazi: mwanamke asili yake ni kimwili zaidi, kihisia zaidi, na mwanaume ana asili ya ubongo zaidi.
Lakini mwanaume anapata usumbufu ule ule anaopata mwanamke anapokuwa kwenye hedhi. Tofauti ni moja tu, kwamba mwanaume hatoki damu. Lakini kila mwezi, baada ya siku 28, hali fulani ya kiakili na kihisia itakuwa inajirudia.
Na kama umejaribu kujichunguza kwa mwaka mzima, utashangaa kwamba, ulikuwa na hasira mgomvi, mwenye huzuni na vingine vya aina hiyo, si hivihivi tu bali ni kwa sababu ulikuwa kwenye hedhi.
Kama ukishafanya zoezi nililokwambia la dayari, jiulize, kama ulipokuwa kwenye hali hizo ulikuwa umekerwa na yeyote au chochote. Utagundua kwamba hukuwa umekerwa bali ulikuwa unasumbuliwa na hedhi yako.
Wanaume na wanawake wanabalehe au kuvunja ungo karibu muda ule ule; umri ambao ni miaka 13. Kwa hiyo kikomo cha kusikia hamu ya ngono hakiwezi kuwa tofauti; kitakuwa miaka 42. Lakini miaka hii 42 inategemea na majaaliwa ya asili.
Kama mwanaume sio mchafu wa kupenda sana ngono, basi miaka 42 hakitakuwa kikomo chake cha kuwa na hamu ya kufanya ngono, ataendelea kuwa na hamu ya kufanya ngono hadi atakapoenda kaburini.
Mwanamke kadhalika kama sio mpenda kufanya ngono kwa fujo naye hamu ya kufanya ngono itandelea hata baada ya kuvuka miaka 42. Vinginevyo kama mwanamke ni mwingi wa mambo, katika umri wa miaka 42 ataacha kuona hedhi yake.
Akishafikisha miaka 42 hamu yake ya kufanya mapenzi inaisha vilevile, katika umri huo huo. Kwamba kila mwanamke anayekoma kuona hedhi kwenye umri huo ni mwingi, hapana.
Mwanaume na mwanamke wameumbwa kwa ‘matofali’ yaleyale, kwa maumbile yaleyale na baiolojia ileile. Tofauti yao ni kwamba mwanaume ni chanya na mwanamke ni hasi kama tungekuwa tunazungumzia umeme.
Huwezi kupata umeme kwa kuwa na chanya mbili; wala ukitumia hasi mbili bali ukichanganya chanya na hisi. Hivyo, kama mwanamke anapata hedhi kama hatua muhimu kuelekea mwito wa kimaumbile, haiwezekani mwanaume asipitie hatua hiyo, ingawa kwa uchanya wake.
Kupata hedhi kwa mwanamke inaeleweka kwamba, ni kutokana na wito wa kimwili. Maana yake ni kwamba, alikuwa amefikia hatua ambapo kimaumbile alitakiwa kujamiiana ili apate ujauzito.
Je, kama hakuna mabadiliko kwa mwanaume, itawezekana vipi mwanaume kujamiiana na mkewe ambaye yuko kwenye hitaji hili la kimaumbile?
Ina maana basi kwamba mwanaume naye ni lazima kila mwezi awe na mabadiliko ambayo yatamfanya aingie mahali ambapo atavutana na mwanamke kimapenzi.
Hili ni suala la maumbile ili kufanya kuzaliana kuwepo. Utajuaje kuwa mwanaume ameingia kwenye hali hiyo? Ndiyo pale ambapo wataalamu wamegundua hizo siku nne au tano za mabadiliko ya kiakili kwa mwanaume

Wasiliana na mwandishi wa  makala hii
Shabani Kaluse Dar es salaam,
Tanzania,
+255 715 729292, au
kwa anuani ya barua pepe: kaluse2008@gmail.com

Friday 21 October 2016

Unene kupita kiasi unachochea kisukari, saratani, kiharusi

Katika baadhi ya tamaduni hasa katika nchi za Afrika, unene unatajwa kuwa ni sifa, ufahari au pengine kipimo cha maisha mazuri. Aghalabu mtu anaponenepa huambiwa hongera au watu humzungumzia kuwa ana maisha mazuri.
Hata hivyo, kiafya ongezeko kubwa la kilo katika mwili wako ni hatua zinazoweza kukusogeza katika mauti.
Shirika la Afya Duniani (WHO) linafafanua kitaalamu kuwa, unene kupita kiasi ni ongezeko la mafuta lisilo la kawaida mwilini linaloweza kuathiri afya.
Takwimu za kidunia kutoka WHO zinaeleza kuwa asilimia 13 ya watu walikuwa na unene kupita kiasi mwaka 2014.
Kati yao asilimia 11 walikuwa wanaume na asilimia 15 walikuwa wanawake. Takwimu za WHO zinasema zaidi kuwa kumekuwa na ongezeko mara mbili ya watu wenye unene kupita kiasi kuanzia mwaka 1980.
Daktari Bingwa wa magonjwa ya binadamu, afya ya familia na vijana, Ali Mzige anasema unene kupita kiasi au kiriba tumbo ni janga la kitaifa na kiashiria cha maradhi yanayoweza kusababisha kifo.
“Katika nchi zinazoendelea unene unasababishwa na mfumo wa maisha, kwa mfano ulaji wa vyakula kama mayai, chipsi vyakula vya kusindikiwa vinasababisha unene huo,” anasema Dk Mzige.
Anasema kuwa unene kupita kiasi ni tatizo kubwa hapa nchini na lisipofanyiwa kazi linaweza kuigharimu nchi kama linavyozigharimu nchi za Magharibi kwa mfano Uingereza.
Kwa mfano Uingereza inatumia Trilioni 1.03 kwa ajili ya kupunguza unene na zaidi ya Dola 150 bilioni kupunguza unene kwa watoto.
“Watoto wanakunywa soda na juisi za kusindikwa, watu hawafanyi mazoezi na hawali mbogamboga na matunda. Ni lazima watapata kiriba tumbo,” anasema.
Anasema kuwa kutokana na unene kupita kiasi, hivi sasa hapa nchini asilimia tisa ya watu wana kisukari, wakati asilimia 25 wana shinikizo la damu. Kadhalika anasema unene unasababisha asilimia 35 ya saratani za aina zote.
“Licha ya hilo, watu milioni 2.7 wanapata saratani kwa kutokula mboga za majani na matunda na kwa kunywa pombe kupita kiasi,” anasema.
Anazungumzia zaidi adha ya unene na kusema kuwa ugonjwa wa saratani unawalenga watu wenye miaka kati ya 30 na 69, lakini hasa kama hawafanyi mazoezi na wanakula vyakula vya mafuta.
Unene sahihi ni upi?
Dk Mzige anasema unene kupita kiasi unabainika pale ambapo mtu ana uwiano usio sahihi wa urefu na unene. Kwa mfano kama mwanamke ambaye hajapata mtoto mwenye urefu wa sentimeta 164 anatakiwa awe na kilo 58. Kwa mwanaume mwenye urefu wa inchi 5 hadi 10 anatakiwa awe na Kilo 68.
“Unene ni janga la kimataifa si kwa hapa nchini, bali hata katika nchi nyingine. Katika baadhi ya nchi hasa jeshini, ukiongezeka uzito hupewi promosheni,” anasema.
Daktari wa Kitengo cha Uchunguzi wa Magonjwa Hospitali ya Muhimbili, Innocent Mosha anasema unene pekee si chanzo cha saratani lakini unene uliozidi husababisha kuzalishwa kwa wingi kwa homoni za oestrogen ambazo husababisha saratani.
“Unene kupita kiasi husababisha kuzalishwa kwa tezi ya androgen, tezi hii hutengeneza kitu kinachoitwa aromatase ambayo husababisha kutengenezwa kwa oestrogen ambayo husababisha saratani,” anasema.
Dk Mosha anasema kila mtu ana seli za saratani lakini mwili wenyewe una mfumo wa kupambana na saratani, endapo mfumo huo utafeli basi saratani huanza kushambulia vimeng’enyo vya aromatase ambavyo hupatikana katika tishu za mwili, ubongo, nyumba ya uzazi, ngozi, mifupa na kimeng’enya hiki ni muhimu katika tendo la ndoa.
Utafiti uliofanywa na Muhihi A. J na wenzake jijini Dar es Salaam mwaka 2013 ulibaini kuwa asilimia 13 ya wanaume wana unene kupita kiasi wakati asilimia 36 ya wanawake walikuwa na tatizo hilo pia.
Kadhalika utafiti huo ulibaini kuwa licha ya Watanzania kuonekana kuwa na unene kupita kiasi, ni asilimia mbili tu ya wanawake walikubali kuwa wana tatizo hilo wakati kwa upande wa wanaume hakuna aliyekubali kuwa na tatizo. Hata hivyo, asilimia 87 ya kundi hilo walikubali kupunguza uzito.
Unene kwa watoto
Dk Mzige anazungumzia suala la unene kwa watoto na kusema kuwa kwa sasa kuna ongezeko kubwa la unene kwa watoto hali inayotishia usalama wa afya zao.
Anasema wazazi wengi hudhani kuwa mtoto mnene ni afya nzuri jambo ambalo anasema ni kinyume chake kwani hicho ni kiashiria cha magonjwa.
“Wazazi wanatakiwa kuelimishwa kuhusu hali hii. Unene si afya njema. Haiwezekani mtoto wa miaka mitano akawa na kilo zaidi ya 20. Hii ni hatari kwa afya yake,” anasema.
Mariam Kishumba, mkazi wa Tandika, Maguruwe anasema akiwa ni mwenye umri wa miaka 35 ana kilo 110 jambo ambalo limemsababishia kupata kisukari.
“Pamoja na kisukari lakini pia nina matatizo ya miguu, nashindwa kupumua vizuri na wakati mwingine mapigo ya moyo yanakwenda kasi,” anasema.
Chanzo cha unene kupita kiasi
Kichocheo cha unene kupita kiasi ni kula vyakula vya wanga vyenye mafuta kupita kiasi. Kukosa mazoezi ya kawaida ya viungo.
WHO inaeleza kuwa kubadilika kwa mfumo wa maisha kama kutembea kwa gari, kula vyakula vya kusindikiwa ndicho chanzo cha unene. Magonjwa mengine yanayoweza kusababishwa na unene kupita kiasi ni pamoja na maradhi ya moyo, kiharusi, magonjwa ambayo yaliongoza kwa kuua mwaka 2012.
Source: Mwananchi

Prepared by Dr Salim Amour 
Cardio_thoracic Surgeon