Search This Blog

Thursday, 10 September 2020

๐‘ฝ๐‘ฐ๐‘ซ๐‘ถ๐‘ต๐‘ซ๐‘จ ๐‘ด๐‘ซ๐‘ถ๐‘ด๐‘ถ๐‘ต๐‘ฐ ๐‘ต๐‘จ ๐‘ป๐‘ฐ๐‘ฉ๐‘จ ๐’€๐‘จ๐‘ฒ๐‘ฌ (๐‘ด๐’๐’–๐’•๐’‰ ๐’–๐’๐’„๐’†๐’“๐’”)

Vidonda vya mdomoni ( Mouth ulcers) huweza kupelekea muhusika kushindwa kufurahia chakula anachokula au hata maongezi nk

Vidonda vya mdomoni huweza kuwa vikubwa au vidogo kulingana na sababu zilizopelekea kidonda hicho , kwa kawaida vidonda hivi hupona kati ya siku 7 hadi 14 . Lakini endapo ni vikubwa huweza kuchukua muda mrefu kupona

๐Ÿ“ค Je , SABABU ZINAZOPELEKEA VIDONDA VYA MDOMONI NI ZIPI?


๐Ÿบ Majeraha wakati wa kusafisha kinywa na majeraha mengine kama yanayosababishwa na ajali au wakati wa kupata huduma za kinywa kwa madaktari wa meno
.
๐Ÿบ Vyakula na asidi iliyomo , mfano Matunda kama limao nk yenye asidi nyingi huweza pia kusababisha vidonda
.
๐Ÿบ Ukosefu wa vitamin B-12, zinc , folate au Iron
.
๐Ÿบ Mabadiliko ya homoni kipindi cha hedhi
.
๐Ÿบ Mzio dhidi ya bacteria wa kinywa
.
๐Ÿบ Matumizi ya braces
.
๐Ÿบ Msongo wa mawazo na ukosefu wa usingizi
.
๐Ÿบ Maambukizi ya bacteria, fungi na virusi


๐Ÿ“ค PIA VIDONDA VYA MDOMONI HUWEZA KUTUELEZA MATATIZO MAKUBWA YANAYOHITAJI MATIBABU YA HARAKA KAMA VILE ;


โ˜” Celiac disease ( Hutokea baada ya mzio wa kinga ya mwili dhidi ya Gluten , kisha villi huathiriwa au kuharibiwa , kiufupi ni tatizo katika mfumo wa chakula , kisha sehemu zingine za mwili pia huathiriwa)
.
โ˜” Inflammatory bowel disease
.
โ˜” Behcets disease
.
โ˜” Kisukari
.
โ˜” Ukimwi
.
โ˜” Kinga ya mwili inaposhambulia seli katika tishu mbalimbali badala ya kushambulia bacteria , au virusi


๐Ÿ“ค HIZI NI NJIA BAADHI YA KUTIBU TATIZO HILI LA VIDONDA VYA MDOMONI ;

โ˜” Sukutua kwa maji ya chumvi au baking soda
.
โ˜” Kuweka (Milk of magnesia ) katika vidonda - Utazipata pharmacy
.
โ˜” Kutumia bonzocaine - Mfamasia atakuelekeza
.
โ˜” Tumia virutubisho vyenye vit B-12 , B-6 , iron, zinc, folic acid


๐Ÿ“ค Zingatia ya fuatayo kuepuka tatizo ;

๐Ÿบ Kama tatizo lilitokana na kutumia sana vyakula au matunda yenye asidi nyingi basi punguza matumizi yake
.
๐Ÿบ Zingatia usafi wa kinywa kila siku
.
๐Ÿบ Kula mlo kamili
.
๐Ÿบ Pata usingizi wa kutosha
.
๐Ÿบ punguza stress

๐Ÿ“ค USHAURI ; Ikiwa vidonda ni vikubwa na unapata maumivu sana , zipo dawa za kupunguza maumivu . Ikiwa una bacterial au viral infection Onana na daktari uanze matibabu , dawa zipo


USIKAE MDA MREFU NA HIVO VIDONDA , MAANA BAADAE ITAKUA NGUMU SANA KUTIBIKA , NA VINAWEZA SABABISHA CANCER , KUNA WATU WANAKAA NA HIVYO VIDONDA KWA MIAKA , NI HATARI

2 comments:

  1. Mimi Nina kinyama mdomoni haliumi Ila kipo MDA mrefu n Kama kiuvimbe tu sijielewi nifanyaj?

    ReplyDelete
  2. The best herpes remedy, email [robinsonbucler@] gmail com

    ReplyDelete

Fitness & Exercise Calculator
Activity
Time (hrs or mins)
Distance
Gender
Height
Weight
Age
Calculate
Computing...