Search This Blog

Saturday, 12 September 2020

TATIZO LA MIPASUKO KATIKA ULIMI

๐Ÿ“š Ulimi wa mtu kwa kawaida hautakiwi kuwa na mipasuko ya aina yoyote . Sasa hawa watu wenye ulimi uliopasuka huwa hawana maumivu , isipokua tu labda kama kuna chakula kimekwama kwenye hiyo mipasuko ndio muhusika atahisi maumivu

๐Ÿ“š Mipasuko hii huweza kuwa iliyochimbika sana au kiasi tu.
Wazee ndio hupatwa sana na hii mipasuko ya ulimi , japo yeyote yule anaweza kuwa na ulimi wa hivi.
Wanaume ndio huwa zaidi na tatizo hili kuliko wanawake

๐Ÿ“ค NINI HUSABABISHA HALI HII ?

Hadi sasa , wataalamu hawajui ni nini hupelekea hali hii ya mipasuko kwenye ulimi , japo ina amini kwamba watu wenye undugu (genetics) huweza kuwa na tatizo hili na wengine wasiwe nalo . mfano katika familia , unaweza kuta mzazi ana tatizo hili na watoto pia
.
Mfano : Kuna tafiti ilifanyika na ikabaini kwamba watu wa South Africa ni 0.6% tu ya watu wote ndio wana tatizo hili la mipasuko kwenye ulimi , lakini Katika Taifa la Israel 30.6% ya watu wote ndio wana hii hali. Sasa unaweza ona kwamba swala la jamii fulani yenye mfanano wa kigenetiki huweza kuwa na hii hali ya mipasuko na jamii nyingine isiwe nayo

๐Ÿ“ค TATIZO HILI LA MIPASUKO KATIKA ULIMI HUWA NA UHUSIANO NA MAMBO KAMA HAYA :

โ˜‚ Geographic tongue

โ˜‚ Kuvimba kwa lips na uso kutokana na matatizo ya neva
.
โ˜‚ Upungufu wa virutubisho muhimu kwa mwili n.k japo hii huwa na mchango mdogo

MATIBABU

Tatizo hili kiufupi , halihitaji tiba , isitoshe kisababishi hakijulikani , .

๐Ÿ“ค USHAURI

Ubaya wa hii mipasuko ni kwamba endapo chakula kitabakia kwenye hiyo mipasuko , itapelekea bacteria kuzaliana , maumivu na hata kupelekea harufu mbaya ya kinywa na hata kuchangia meno kuharibika


Muhusika pia anakua katika mazingira marahisi ya kushambuliwa na fungus wa kinywa (candinda ablicans) , ikiwa imekutokea basi dawa zipo , onana na daktari


๐Ÿ“š Hakikisha unafanya usafi wa kinywa angalau mara mbili kila siku , na uwe na utaratibu wa kumuona daktari wa meno angalau mara mbili kwa mwaka


MWISHO NA ASANTENI ๐Ÿ™

1 comment:

  1. Am facing the same problem how can I get the medicines

    ReplyDelete

Fitness & Exercise Calculator
Activity
Time (hrs or mins)
Distance
Gender
Height
Weight
Age
Calculate
Computing...