Search This Blog

Wednesday 17 May 2017

MENO YAWE MEUPE NA MUONEKANO BOMBA


Meno ni kiungo cha ajabu sana ambapo kinapokua na muonekano mzuri hukufanya uwe na furaha na tabasamu zito mbele ya wenziwako. Na kinyume chake mtu hukosa kujiamini mbele za watu na tabasamu la dhati hutoweka. Hivyo nimeona ipo haja ya kukuainishia kwa mukhtasari njia anuai za Kung'arisha meno yako na kukufanya ujiamini katika mazungumzo.

[​IMG]


Meno kuwa ya manjano(discolouration) huchangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya vyakula tulavyo, matumizi Ya vinywaji vya viwandani ambavyo huaribu kabisa meno yako. Lakini pia namna ya kupiga mswaki huchangia hilo, hivyo ni vema kuzingatia kanuni sahihi za upigaji wa mswaki.



Meno kuwa na rangi ya kahawiya hii husababishwa na aina ya maji kutokana na aina ya miamba ya sehemu husika .mfano uzoefu unaonesha maji yenye kiwango kikubwa cha madini ya fluoride huchangia meno kupoteza rangi yake ya asili , Matumizi ya sigara, tumbaku,unywaji wa kahawa kupita kiasi.



Hizi hapa ni njia mbadala za kufanya meno yako kuwa meupe na mvuto;



Baking soda .sodabiki,au maarifu kama unga wa soda. chukua nusu kijiko cha baking soda pigia mswaki, au weka pamoja na matone kadhaa ya limau, au maji ya limau ya vuguvugu. Pigia mswaki.hii husaidia sana Kung'arisha meno kutokana na Tahiti za wadau wa afya. Lakini ni vema kutumia kwa uangalifu, yaani mtu asizidishe zaidi ya Mara tatu kwa wiki,

[​IMG]


Maganda ya ndizi za kuiva (banana peels). Unaweza kusugua meno yako kwa kutumia maganda ya ndizi, maganda ya ndizi yana madini kama magniziam, potasiam, na manganese, hivyo husaidia kutakatisha meno yako. Sugua meno yako kwa maganda ya ndizi kisha acha kwa dakika angalau Milo na uendelee kupiga mswaki wako kama kawaida .



Kutafuna karoti, jitahidi kutafuna karoti kwa wingi mno kwani husaidia kufanya meno yako yawe meupe na mvuto bomba.




Matumizi ya bizari (turmeric), bizari hutumiwa kama kiungo katika jamii nyingi za upwa wa afrika mashariki. Lakini pia tafiti zinaonesha kuwa hutakatisha meno yetu. Ni vizuri ukaongezea na juisi ya limau kidogo na kuutumia mchanganyiko huu .
[​IMG]



Mafuta, unaweza pia kusugua meno yako kwa kutumia mafuta ya mzaituni (olive oil), au mafuta ya ufuta (sesame oil) au mafuta ya halizeti (sunflower oil) .namna ya kutumia chukua kijiko kimoja cha mafuta husika na sugua meno yako ,kisha piga mswaki wako kama ada ,pia unaweza kutumia mafuta ya nazi husaidia mno


[​IMG]


Limau, unaweza kusugua meno yako kwa kutumia maganda ya limau, au kutumia maji ya limau au kutumia dawa za mswaki zenye limau ndani yake.

[​IMG]
[​IMG]

Matumizi ya karafuu(cloves), hii uboresha harufu ya kinywa, kuuwa vijidudu kinywani na kulinda vizi na meno kwa ujumla
[​IMG]

Ahsanteni kwa kufuatilia makala zangu.

1 comment:

  1. The best herpes remedy, email [robinsonbucler@] gmail com

    ReplyDelete