Bawasiri hutokea pale mishipa ya damu inapovimba au kuathiriwa kutokana na mgandamizo unaotokea katika sehemu ya chini ya puru.
Kuna aina mbili ambazo ni :๐ Bawasiri ya nje ; Hii hutokea ndani ya ngozi lakini katika sehemu ya nje ya tundu la haja kubwa (Anus)
.
๐ Bawasiri ya ndani : Hii hutokea katika kuta za njia ya haja kubwa kwa ndani.
๐ค Nini husababisha Bawasiri ?
Tatizo hili hutokea pale kunapokua na mgandamizo mkubwa katika mishipa ya damu (Veins) kuzunguka eneo la tundu la haja kubwa
Hili huweza sababishwa na mambo yafuatayo :
โ Kukaa chooni kwa muda mrefu
.
โ Tatizo la kuwa na haja kubwa ngumu kwa muda mrefu
.
โKuharisha sana kwa muda mrefu
.
โ Kula vyakula visivyokua na nyuzinyuzi
.
โ Kulegea kwa tishu maeneo ya tundu la haja kubwa (Hili husababishwa na swala zima la uzee au ujauzito )
.
โ Kunyanyua vitu vizito mara kwa mara
๐คJe , Dalili ni zipi ?
BAWASIRI YA NJE :
โ Muwasho katika tundu la haja kubwa
.
โ Uvimbe mmoja au zaidi pembezoni mwa tundu la haja kubwa
.
โ Maumivu ya njia ya haja kubwa , hasa wakati wa kukaa
Swala la kujisafisha au kujikuna mara kwa mara kutaongeza tatizo liwe kubwa zaidi. Hali hii huweza kuisha ndani ya siku chache
BAWASIRI YA NDANI :
โ Damu kutoka katika njia ya haja kubwa , hasa wakati wa kujisafisha au wakati wa kujisaidia
.
โ Maumivu utayasikia wakati wa haja au unapobanwa na haja kubwa. Mara nyingi ni ngumu sana kuhisi maumivu hadi sehemu iliyoathirika itoke nje ya tundu la haja kubwa , yani kama kinyama hivi kutoka ndani ya puru
๐คJe, Nikiwa nyumbani nawezaje kujitibu ?
โ Kula vyakula vyenye nyuzi nyuzi
โ Tumia dawa za kulainisha haja kubwa au virutubisho vyenye nyuzi nyuzi ( Fiber suppliments )
โ Kunywa maji ya kutosha kila siku
โ Usitumie nguvu kubwa kujisukuma wakati wa haja kubwa
โ Usikae chooni muda mrefu (Hasa vile vyoo vya kukalia)
โ Tumia dawa za kupunguza maumivu
.
โ Chukua maji ya vuguvugu , yaweke kwenye beseni kisha utayakalia kwa dakika kadhaa , lakini unapoyakalia usikalie beseni yani njia ya haja kubwa ikusane na maji tu.
No comments:
Post a Comment